
Kwenye
Jamhuri Rais ana mamlaka makubwa sana, Hivyo, kwenye Jamhuri, Rais aweza
kuwa dikteta, akitaka. Anaweza kuonea na hata kukandamiza raia wake.
Kuwanyima haki.
Kwenye
nchi yetu hatujapata bahati mbaya ya kuwa na Rais dikteta. Na hata wale
wenye kutamani Rais dikteta, kimsingi hawajawahi kuishi kwenye utawala
wa rais dikteta.
Na
yanayoitwa maamuzi magumu ya Rais kwenye Jamhuri yaweza pia kutafsiriwa
kama maamuzi ya kidikteta. Kinachotakiwa ni maamuzi yenye hekima na
busara. Na mwenye kutanguliza hayo, maamuzi yake husemwa pia kuwa ni
magumu. Maana, si kazi rahisi kufikia maamuzi yenye hekima na busara.
Maamuzi yenye kuzingatia Utu na Haki.
Rais
kwenye Jamhuri anapaswa kuwa kielelezo cha Utu na Haki. Maana, Rais
kwenye Jamhuri yumkini ni kimbilio la mwisho la mnyonge, na mwenye nguvu
pia. Ni kwenye kudai haki yake anapoona ameikosa kwengineko.
Kwenye
utawala wake, Mzee Ali Hassan Mwinyi alianzisha utaratibu wa kukutana na
wananchi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi kwenye ofisi ndogo za CCM,
Lumumba. Mzee Mwinyi alitambua, kuwa miongoni mwa aliowaongoza, kuna
wanyonge na hata wenye nguvu, waliokoseshwa haki zao kwenye mifumo ya
kawaida, na hawakuwa na pakukimbilia, isipokuwa kwa Rais wa Nchi.
Ndio,
kwenye Ikulu za Afrika, zenye kukaliwa na Marais wenye kuthamini Utu na
Haki za raia wao, kila kukicha, utawakuta raia, wengine wamesafiri
kutoka umbali mrefu, wametaka waelekezwe iliko Ikulu, ili wao wenyewe,
wamfikishie Rais kero zao.
Ndio maana ya kusema, Katika Nchi, Rais ni kielelezo cha Utu na Haki.
Ni Neno La Leo.
Maggid,
Mji Mkongwe, Zanzibar.
Maggid,
Mji Mkongwe, Zanzibar.