THE DREAM STUDIOS

wambura babu log

DARDYS FASHION

DARDYS FASHION

Monday, 22 December 2014

MH. PINDA AKUTANA NA WATANZANIA WAISHIO QATAR


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Mama Tunu Pinda wakizungumza na Mchezaji Mwinyi Kazimoto ambaye ni Mtanzania anayecheza soka la kulipwa katika timu ya Al Markhiaya nchini Qatar, katika mkutano kati yake na watanzania waishio nchini humo uliofanyika kwenye hoteli ya Sheraton mjini Doha Desemba 21, 2014.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na mkewe Mama Tunu Pinda (kushoto kwake) wakizungumza na baadhi ya washiriki wa mkutano kati yake na watanzania waishio nchini Qatar uliofanyika kwenye hoteli ya Sheraton iliyopo Doha, Desemba 21, 2014.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja na watanzania waishio nchini Qatar baada ya kuzungumza nao kwenye hoteli ya Sheraton iliyopo Doha, Desemba 21, 2014.